Monday, June 30, 2014

UKATILI! Mwanamke auawa kwa wivu wa mapenzi huko Mpanda

By on 7:03 AM

MWANAMKE mmoja   aliyefahamika kuwa ni Cesilia  Clementi (22) Mkazi wa Mtaa wa Majengo B Mjini Mpanda ameuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake na mpenzi wake aliyefahamika kwa jina moja la Kanu ambaye ni mfanyabiashara wa Mpunga  wa kutoka mkoani Kigoma.
Kwa mujibu wa Kamanda polisi mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari, tukio hilo la mauaji ya kusikikisha ya mwanamke huyo limetokea hapo jana  saa mbili asubuhi nyumbani  kwa  shemeji ya marehemu aitwaye Mashaka Hanja  katika Mtaa  huo wa majengo mjini hapa
Alisema kuwa kabla ya tukio hilo marehemu ambaye alikuwa akiishi kwa dada yake mke wa Mashaka Hanja  walikuwa wanamahusiano ya  kimapenzi  na mpangaji wa nyumba hiyo, ambapo  aliamka asubuhi na kuanza kufagia nje ya nyumba hiyo.
Wakati akiwa anaendelea kufagia ndipo Kanu alitoka ndani na kumwita mpenzi wake huyo na kisha waliingia ndani ya chumba alichokuwa wakiishi ghafla majirani walianza kusikia marehemu akishutumiwa na  Kanu kuwa siku hizi hamjali kwa kuwa ameisha  pata mwanaume mwingine.
Walieleza  baada ya mabishano ya muda mfupi walisikia  marehemu akipiga mayowe   ya kuomba msaada na majirani hao walipojaribu kufungua mlango  walishindwa kwani ulikuwa umefungwa kwa ndani
Aliongeza kuwa majirani hao walijaribu kumsihi Kanu afungue mlango lakini hakufanya hivyo   hali ambayo iliwalazimu wachungulie dirishani na  kumwaona Kanu akimchoma marehemu na  kisu  kwenye sehemu mbalimbali za mwili wake.
Polisi walipata taarifa hizo    na mara walifika kwenye eneo hilo huku wakiwa na silaha na kuweza kuvunja mlango na walipoingia ndani walikuta marehemu akiwa ameishafariki dunia huku mwili wake ukiwa unagalagala chini ya sakafu
Na Kanu akiwa hoi huku na hana fahamu baada ya kuona amemuua mpenzi wake na yeye kuamua  kujichoma kisu katika sehemu ya tumbo  na shingoni
Jeshi la polisi   Mkoa wa Katavi limethibitisha kutokea kwa mauaji ya mwanamke huyo na wanamshikilia mtuhumiwa huyo huku akiwa amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda  

0 comments:

Post a Comment