Saturday, October 4, 2014

By on 6:08 AM

Alarm over deforestation



Morogoro. More than 200, 000 hectares of forests are cleared annually for charcoal production, The Citizen has learnt.
This is so because over 90 per cent of Tanzanians use charcoal as a major domestic energy source.
The concern was raised by Rural Energy Agency (Rea) consultant Shima Sago, when closing a training on alternative charcoal production.
The alternative charcoal is made from remains of plants such as shells of coconuts, corn, rice husks and wood waste.
The consultant told The Citizen that the training was provided to a group of 18 people from Kiswila Village, Matombo Division in Morogoro District.
He said the training was aimed at equipping participants with skills of producing alternative charcoal for their households use as well as for selling to other community members.
Mr Sago said apart from helping to conserve the environment, engaging in producing alternative charcoal would ensure appropriate utilisation of plant remains that are used as raw materials for domestic energy.
He also said the charcoal would boost the economies of most households as the alternative domestic energy source is more efficient than the traditional wood charcoal.
“Households will now be capable of using a very small amount of charcoal given its efficiency,” he said.
For her part, Morogoro Municipal community development officer, Ms Monica Lindi, expressed her optimism, saying the environmentally friendly technology would raise the income of most communities.
She advised the training participants to teach others who did not get the opportunity to attend.
“You should act as ambassadors by passing the skills you have gained to other community members, particularly women who are in most cases responsible for searching for household energy sources,” she told the participants.

Selous anti-poaching drive pays off

By on 6:06 AM


Minister for Natural Resources and Tourism Lazaro Nyalandu. PHOTO|FILE 
By Bernard Lugongo,The Citizen Reporter


Dar es Salaam. Minister for Natural Resources and Tourism Lazaro Nyalandu has announced success in fighting poaching as the country has recorded zero elephant killing in the Selous Game Reserve in the past three months. 
Mr Nyalandu, who spoke at the climax of the Swahili Tourism Expo in Dar es Salaam on Thursday evening, commended game rangers and other stakeholders who have given their lives to protect the wild animals in the area.
In June, the World Heritage Committee meeting held in Doha (Qatar) inscribed the Selous Game Reserve on the List of World Heritages in Danger because widespread poaching was decimating wildlife populations in the reserve.
“We will not get tired, the battle is not won yet,” he said as participants clapped and cheered.
Statistics show that poachers are killing the elephants for their ivory at alarming rates that the population could be completely wiped out in just six years.
Tanzania’s Elephant Protection Society said that about 30 elephants are killed daily, and at this rate the population will be exterminated by 2020. 
At the Selous Game Reserve, rampant poaching has caused a dramatic decline in wildlife populations, especially elephants and rhino, whose numbers have dropped by almost 90 per cent since 1982, when the game reserve was inscribed on the World Heritage List.
Covering 50,000 square kilometres, the Selous Game Reserve is one of the largest protected areas in Africa.
Mr Nyalandu said that he was looking forward to seeing the tourism industry stabilize by increasing the number of wild animals and tourists coming to Tanzania, to make the sector sustainable.
He assured tourist companies of not introducing new fees in the sector without properly consulting them on the matter.

Sunday, August 31, 2014

Pombe Sio Chai Jamaa Bia Mbili Tu Kaanza Kuvua Nguo na Kuweka Mapozi ya Kimisi Watu Wampige Picha

By on 5:00 AM


Pombe usipoweza kuicontrol basi matokeo yake ita Control wewe ! Huyu Jamaa Alinawa na Kamera za Udaku Specially Katika Baa Moja Maarufu Mitaa ya Sinza , Inasemekana Alikuwa na Wenzake wanakunywa Baada ya Kupata Bia Mbili tu zikampanda Kichwani na Kuanza kuweka Mapozi ya Ajabu Ajabu na Mwisho Kuvua nguo na kuweka Mapozi ya Kimiss Watu Wampige Picha, Wenzake kuona Hivyo Wakamkimbia na Kumwacha Mchizi akiabika Kiaina..

Friday, August 29, 2014

Ajinyonga shambani na kuacha ujumbe; “Nawaachia dunia yenu muishi miaka 110”

By on 10:14 PM

Mtu mmoja ambaye hakujulikana jina, amekutwa akiwa amejinyonga ndani ya kibanda shambani huku akiwa na karatasi iliyoandikwa ujumbe “Nawaachia dunia yenu muishi miaka 110”
Mwenyekiti wa Kijiji cha Kibiki, Ally Hussein alisema kijana huyo mwanamume amekutwa saa mbili usiku akiwa amefariki na hivyo kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi Chalinze.
Alisema askari walifika na kuukuta mwili wa marehemu ukiwa umefungwa kamba ya katani na alipopekuliwa alikutwa mfukoni na karatasi yenye maandishi hayo.
Kaimu Kamanda wa Polisi Pwani, Mrakibu msaidizi, Athumani Mwambalaswa amethibitisha tukio hilo na kusema mwili wa marehemu ulichukuliwa na kuifadhiwa Kituo cha Afya Chalinze kusubiri uchunguzi wa daktari.
shambani
Hata hivyo, alisema bado haijafahamika mtu huyo ni mwenyeji wa kijiji kipi kwani hapo Kibiki hakuweza kutambulika na jitihada za kutafuta ndugu zake katika vijiji vya jirani zinafanyika. Chanzo cha kujinyonga bado hakijajulikana

Sitta Awajibu Wanaofananisha Tume Ya Warioba na Bunge la Katiba

By on 10:08 PM

 Baada ya watu na taasisi kadhaa kudai kitendo cha Bunge Maalumu la Katiba kupokea maoni ya wananchi na kuyaongeza kwenye rasimu ya Katiba mpya, ni kuingilia kazi ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samwel Sitta, alisema bunge hilo lina mamlaka makubwa kuliko tume hiyo.
 
Amesema hata wajumbe wa bunge hilo wanaoendelea kupitia rasimu hiyo, siyo mazuzu, wana akili zao, wasomi na wapo watu wengi wanaotambua kazi hiyo na kuipongeza. 
 
Sitta alivunja ukimya huo na kutoa ufafanuzi jana mbele ya
waandishi wa habari kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma, na kuongeza kuwa wananchi wameona rasimu ya Katiba mpya, ina upungufu.
 
“Mimi naelewa kuna watu wanakasirishwa sana na kazi tunayoendelea kuifanya, ni haki yao kukasirika lakini kinachofanywa ni wananchi ambao hatukuwaalika, wanakuja kwa makundi kuelezea wanachoona kuwa ni upungufu ndani ya rasimu, sasa haya watayapeleka wapi? 
 
“Hii hali ya kuonekana sisi Bunge na Tume tupo hadhi moja si kweli, Tume ina mamlaka yake lakini Bunge lina mamlaka makubwa zaidi ya Tume… waliotunga sheria waliona ipo kazi inayofanyika pamoja na kufanya marekebisho ndio maana wanachotoa wao ni rasimu sisi tutakachotoa inaitwa Katiba inayopendekezwa.”
Alisema dhana kwamba lolote likifanywa kwenye rasimu ni usaliti kwa nchi au inachakachuliwa, msingi wake ni ghadhabu za mtu na uamuzi tu wa kuwaona waliopo Dodoma ni mazuzu.
 
“Hapa kuna watu wasomi wazuri tu wenye akili zao. Kusema tunafanya kazi ya Tume ni upotoshaji mwingine wa watu wasiotakia mema Bunge Maalumu la Katiba. Sijui kwa nini rasimu inapewa hadhi kama msahafu, wakati imeandikwa na binadamu tu ina upungufu mkubwa. 
sitta
 
“Mtaona kuanzia Septemba 2 mijadala ya hoja itakavyokuwa.
Wananchi wao wameona Tume haikuwatendea haki maoni yao waliyoyatoa, na waliona mahali pa kwenda kwenye chombo cha juu zaidi nacho ni Bunge Maalumu la Katiba, tuna wajibu wa kuwapokea kwani tupo kwenye kazi ya kutunga Katiba”. 
 
Alisema kazi inayofanyika, ni kutoa Katiba rafiki kwa wananchi na kutoa mfano wa wasanii, ambao waliona pamoja na kutoa maoni kwa maandishi, hayakuzingatiwa na Tume lakini Bunge kwa vigezo vyake, limeona inastahili.
 
“Wamekuja wakitaka kwenye rasimu kuwekwe kipengele cha mali isiyoshikika, yaani haki miliki bunifu nasi tumeona inastahili, lakini Tume waliiacha nasi tumeongezea kwenye sehemu rasimu iliyoweka mali tu,” alisema. 
 
Miongoni mwa vipengele vilivyoongezwa kwenye rasimu hiyo, ni masuala ya Serikali za Mitaa, yaliyotokana na andiko la aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, ambayo yalipangwa kuwepo kwenye Katiba ya Serikali ya Tanganyika, ambayo ni ardhi, mazingira, rasilimali za Taifa na haki za watumiaji wa bidhaa. 
 
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kamati Namba Moja, Ummy Mwalimu, alisema Kamati yake imeshapitisha sura zote kwa kupata theluthi mbili kila upande, lakini suala la akaunti ya pamoja kwa Tanzania Bara na Zanzibar, hawakufanya uamuzi. 
 
Alisema wajumbe wa kamati hiyo, walitaka suala hilo liwekwe kiporo hadi baada ya kukamilika kwa semina ya wataalamu wa masuala ya fedha, waliokuwa wakiwapa jana kuhusu mgawanyo huo wa fedha. 
 
“Tunataka tujue kwa sasa hali ikoje, changamoto zake na wapi kwenye kero. Kwenye suala hili wajumbe walibishana sana na waliweka pembeni itikadi za vyama vyao vya siasa,” alisema. 
 
Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati Namba 11, Hamad Masauni Yusuf, alisema Kamati yake imeshapiga kura kwenye sura zote na changamoto kubwa waliyokumbana nayo, ni suala la fedha za pamoja. 
 
“Leo (jana) tunategemea kupata elimu kutoka kwa wataalamu wa fedha na tukiona kuna mambo muhimu, itatubidi tuitishe kikao cha dharura kufanya marekebisho. Lengo ni pamoja na masuala ya fedha. Pia Muungano uimarishwe na kusiwe na mambo ya kuutatiza na pande zote mbili zifaidike,” alisema. 
 
Mwenyekiti Kamati Namba Nne, Christopher ole Sendeka, ambaye hakuwepo kwa muda mrefu kuhudhuria kamati kutokana na kuuguliwa na watu wa familia yake, alisema kutokuwepo kwake hakupaswi kuonekana kuwa anaunga mkono Ukawa. 
 
Alisema kwenye kamati yake kulikuwa na mjadala mkali na watu walikuwa wakali lakini mwishowe walielewana vizuri. 
 
Alitaja maeneo yaliyosababisha wajumbe kuwa wakali kuwa ni ardhi, uraia pacha, masuala ya wakulima na wafugaji na muundo wa Bunge. 
 
Mwenyekiti wa Kamati Namba Tatu, Dk Francis Michael, alisema kwenye Kamati yake walipingana sana na kuvutana na kufanikiwa kupata makubaliano mazuri na kila sura kupata theluthi mbili kwenye sura zote.

SMS za Usagaji za Aunt Lulu Zanaswa…Zilikuwa zinaenda kwa binti wa kidato cha pili

By on 9:50 PM
Mama mmoja mkazi wa Sinza jijini Dar es Salaam, aliyejitambulisha kwa jina la Mama Zahara, ameibuka na madai mazito akimtuhumu msanii wa filamu ambaye pia ni mjasiriamali, Lulu Mathias Semagongo ‘Anti Lulu’ kumtumia ‘SMS’ za usagaji mwanaye aitwaye Zahara  ambaye ni denti wa kidato cha pili.

MSIKIE MAMA MWENYEWE

Akizungumza kwa hasira, Mama Zahara aliwaka: “Mimi nina mtoto huyu tu wa kike, anasoma boarding huko Tanga lakini hivi karibuni alirejea akidai wamepewa likizo ya wiki moja.
 
“Tangu huyu mtoto amekwenda boarding, nimebaini amebadilika sana, amekuwa na vijitabia ambavyo sivielewi hivyo nikawa namchunguza sana.
 
“Leo (Jumanne wiki hii) wakati niko jikoni nikasikia anaongea na mtu akiwa chumbani kwake, mazungumzo yale yalinitia shaka kwani kuna muda nikamsikia ‘akimkisi’ aliyekuwa anazungumza naye.
Msanii wa filamu za Kibongo Lulu Mathias.
Msanii wa filamu za Kibongo Lulu Mathias.
“Nilihisi kitu f’lani lakini nikasema nitamvizia nichukue simu yake nikiamini kama kuna kinachoendelea nitagundua, na kweli, alipotoka kwenda bafuni nikaichukua simu yake na kukutana na mambo ya ajabu.
 
“Nilinasa hizi sms ambazo zilinionesha waziwazi kwamba mwanangu anafanya vitendo vya kisagaji. Niliumia sana hasa ukichukulia kwamba nina binti huyo tu.

“Nilipoichukua ile namba, nikataka kujua kama kweli alikuwa anachati na msichana mwenzake au mwanaume, ikabidi nifanye kama nataka kumtumia pesa kwenye simu yake na hapo ndipo likaja jina la Lulu Semagongo.
 
“Nilishtuka kwani namjua huyu msanii tangu alipokuwa mtangazaji. Nilipompigia akanijibu kwa kifupi tu kwamba nimlee vizuri mwanangu na yeye hawezi kumfanyia vitendo hivyo, nikaona bora nije kwenu mtanisaidia.”

MESEJI ZENYEWE ZIKOJE?

Zahara: Natamani kufanya kale kamchezo, unaweza kunisaidia?
Anti Lulu: Nitumie pesa!
Zahara: Kiasi gani cha pesa? Pesa siyo tatizo, umenielewa lakini? Nataka tu…(kitendo kichafu).
 
Anti Lulu: Nitumie hiyohiyo, kwa muda huu nitumie 30,000.
Zahara: Sawa halafu tunaonana vipi?
 
Anti Lulu: Nitumie pesa muda huu, Jumamosi.
Zahara: Mbona mbali sana mpenzi, leo haiwezekani au hata kesho, pesa siyo tatizo.
 
Anti Lulu: Nitumie pesa basi.
Zahara: Subiri kidogo baby, simu yenye pesa iko kwenye chaji, usijali, nashukuru kwa kunionea huruma.
Anti Lulu: (kimya).

KESHO YAKE

Anti Lulu: Umeona ishu kunidanganya siyo?
Zahara: Siwezi kukudanganya mpenzi, ndiyo naamka nitakutumia ila usije ukanidanganya maana nina…, hiyo Jumamosi tunaonana wapi?
 
Anti Lulu: Tuta-meet (kukutana) Bondeni Hotel (ipo Magomeni, Dar), basi nitumie hiyo pesa.
Zahara: Nikutumie kwenye namba hii, vipi tutatumia vifaa?
 
Anti Lulu: Nitumie kwenye namba hii.
Zahara: Nijibu basi kama tutatumia vifaa au hivihivi…
 
Anti Lulu: Hakuna haja ya vifaa, mimi natosha…
Zahara: Haya natuma, nitafurahi sana.
 
Baada ya maelezo ya mama huyo kisha kuziona sms hizo, kweli zilionesha Zahara ndiye aliyekuwa akimshawishi Anti Lulu amfanyie kamchezo hako huku msanii huyo naye akionesha kuujua na kutaka apewe kwanza Sh. 30,000, Ijumaa lilimsaka Anti Lulu ili kupata maelezo yake ambapo alikuwa na haya ya kusema:

HUYU HAPA ANTI LULU

“Kusema ukweli huyo binti ndiye aliyekuwa akinisumbua kwa kunitumia sms za kunitaka.
 
“Alionekana kuuzoea na kuupenda sana sana huo mchezo, mimi sijawahi, ni two different things (vitu viwili tofauti).
 
“Inavyoonekana alitaka kunichafua kwani alinilazimisha sana, sijawahi kufanya huo mchezo na wala sifikirii hasa kwa binti kama mimi ambaye naamini wapo wanaume wanaonipenda, niingie kwenye usagaji natafuta nini?

“Huyo binti mwambieni anikome kabisa.”
 
Chanzo: Gazeti la Ijumaa/gpl

Rais Kikwete: Kuinua Maisha ya Watanzania Sio Kumwaga Fedha Mifukoni

By on 9:42 PM

Rais Jakaya Kikwete amesema dhamira ya Serikali ni kuinua maisha ya Watanzania na dhamira hiyo iko pale pale na kwamba wanaofikiri nia hiyo ni kuwajaza wao fedha mifukoni uwezo huo haupo.
 
Rais alitoa kauli hiyo jana katika Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma wakati akizindua ujenzi wa barabara ya Mbande  hadi Kongwa, itakayojengwa kwa kiwango cha lami.
 
Alisema dhamira ya Serikali ya kuinua maisha ya Watanzania haina maana kuwa wananchi watapewa fedha za kuweka mifukoni mwao.
 
Alisema dhamira ya kuwaletea wananchi maendeleo itafikiwa kwa kupitia uboreshaji wa miundombinu mbalimbali ikiwemo barabara, shule, njia za mawasiliano ili kurahisisha kuweza kufikia malengo yao.
 
“Wengine tunaposema kuinua maisha ya Watanzania wanafikiri ni kumwaga fedha mifukoni mwao uwezo haupo,” alisema.
 
Pia alisema Serikali  imeboresha ukusanyaji wa fedha za ndani ili kuongeza mapato na kuondoa utegemezi katika miradi ya maendeleo.
 
Rais Kikwete alisema makusanyo ya mapato yameongeka kutoka bilioni 170 kwa mwezi hadi bilioni 900 kwa mwezi hivi sasa na ongezeko la fedha hizo linasaidia ujenzi wa barabara za viwango vya lami na hata zile za vijijini.
 
Aidha alisema Serikali inafikiria  kuongeza barabara za lami mbili au tatu za ndani katika wilaya hiyo ya Kongwa.
 
“Tumetimiza ahadi kwenye maeneo mengi  na tunaahidi kuendeleza uwekezaji kwenye barabara, umeme na maji,” alisema.
 
Waziri wa Ujenzi Dk John Magufuli alisema mradi wa barabara kutoka Mbande  hadi Kongwa ni moja ya ahadi katika ilani ya CCM.
kikwete
 
Alisema sehemu ya ujenzi wa barabara hiyo iliyozinduliwa ni kielelezo tosha kuwa serikali imedhamiria kujenga barabara kwa ajili ya kuwaletea wananchi wake maendeleo.
 
“Barabara hii imezinduliwa na Rais ambaye anatoka CCM na mnatakiwa kuhakikisha Rais ajaye anatoka CCM ili aendeleze kazi iliyoanzishwa, haiwezekani barabara hii ije kufunguliwa na Rais wa kutoka chama kingine,” alisema.
 
Alisema barabara nyingi zinajengwa kwa kutumia fedha za ndani kwa asilimia 100 bila kutegemea wafadhili.
 
 “Tanzania ni moja ya nchi zinazojengwa barabara zenye viwango vya ndani kwa kutumia fedha zake za ndani,” alisema.
 
Alisema Serikali itatoa bilioni moja kwa ajli ya kusaidia ujenzi wa barabara za vijijini katika Wilaya ya Kongwa.
 
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Nchini (Tanroads) Mhandisi Patrick Mfugale alisema barabara iliyozinduliwa ni sehemu ya barabara yenye urefu wa kilometa 101.7 ya kutoka Mbande hadi Kibakwe.
 
Alisema ujenzi wa barabara iliyozinduliwa yenye urefu wa kilometa tano asilimia 85 ya kazi yote imekamilika.

Utafiti: Wanawake Wanene ni Mafundi Jikoni Kuliko Wembamba

By on 9:16 PM

Duniani kuna tafiti nyingi na mara nyingi wataalamu wa masuala mabalimbali huja na tafiti tofauti tofauti...

Moja ya tafiti ambayo imenivutia kiasi cha kuja hapa jamvini ni utofauti wa ufundi wa jikoni baina ya mwanamke kimbaumbau na yule mwenye neema za allah "curvaceous" ...

Inaaminika kwamba manawake wenye nyama za nyongeza 'curvy girls' wana ujuzi mkubwa wa mapishi kuwazidi wale ambao miili yao ni vimbaumbau...

Sababu kubwa haswa inayopelekea kuwepo kwa dhana hii ni kutokana na utofauti wa tabia za ulaji baina ya mwanamke tipwatipwa na kimbaumbau...

Wataalamu wanadai eti kwa kuwa wanawake vimbaumbau ni wavivu sana kula basi hata ujuzi wao wa kuandaa madikodiko, mahanjumati na mazagazaga ni mdogo pia...(hawa nafikiri ndio wale wanaochemsha nazi bila hata kuikuna)...

Hivyo wito wangu kwetu vidume haswa wale mnaotafuta waifu matirio, kama wewe ni mtu wa kuchunuku zagazaga hebu konsida basi hiki kigezo usijekuwa walazwa na njaa au kutwa washinda kwa mama muuza...

Mbowe: Mimi ni Kisiki cha CHADEMA

By on 9:05 PM

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe jana alikabidhiwa fomu na makada wa chama hicho na kumtaka awanie tena kiti hicho, ombi ambalo alilikubali na kufungua milango kwa wanachama wengine ‘kupimana naye kifua’. 
“Nafasi bado ipo, anayetaka kupima kifua na mimi ajitokeze. Tena nawaomba viongozi wangu msizuie fomu kwa anayetaka,” alisema Mbowe ambaye ameongoza chama hicho kwa vipindi viwili vya miaka mitano mitano.
Makada wa chama hicho kutoka maeneo mbalimbali nchini wakiongozwa na kada maarufu, Athuman Mzigo (Mapigo Saba) kutoka Kigoma, walikutana na Mbowe na kuwasilisha maombi yao ya kumtaka awanie tena nafasi hiyo.
“Kutokana na sifa za mwenyekiti wetu, tumechangishana Sh200 kila mmoja hadi zikafika Sh50,000,” alisema Mapigo Saba huku akishangiliwa na makada wenzake alioambatana nao na kuongeza:
“Tumemwomba mwenyekiti agombee nafasi hiyo kwa kuzingatia sifa; kwanza anaijua vizuri idadi ya Watanzania na matatizo yao, pili anaungwa mkono na watu wengi na amekisaidia chama kukua. Tulikuwa na madiwani 40 leo wamefika 500, wabunge watano leo 48. Halafu hana ubaguzi ndiyo maana ameunganisha vyama vya upinzani na kuunda Ukawa (Umoja wa Katiba ya Wananchi).”
Huku akichomekea maneno ya lugha ya Kiha, Mapigo Saba alisema kuwa maombi ya kumtaka Mbowe agombee pia yametolewa katika mikoa ya Rukwa, Manyara, Iringa, Njombe, Jimbo la Same Magharibi, Zanzibar, Mwanza na Kilimanjaro.
mbowe
Hotuba ya Mapigo Saba ilifuatiwa na salamu kutoka kwa wazee wa wilaya za Kinondoni, Ilala na Temeke, Baraza la Wanawake (Bawacha) na Baraza la Vijana (Bavicha).
Akitoa salamu za Bavicha, mwenyekiti wa baraza hilo Njombe, Emmanuel Masonga alisema Mbowe ni sawa na Joshua aliyemalizia kuwaongoza wana wa Israel kuingia nchi ya Kanaani:
“Sisi Wakristo tunajua kuwa Mussa alianzisha safari ya Waisrael kwenda Kanaani, ila hakuwafikisha. Kina Mtei (Edwin), Kimesera (Victor), Bob Makani na wengineo walianzisha safari ya kwenda Ikulu, ila hawakutufikisha. Mbowe ni sawa na Joshua atakayetufikisha Ikulu,” alisema Masonga.
Mwenyekiti wa Bawacha Taifa, Susan Lymo alimsifu Mbowe akisema ameongeza hamasa ya wanawake kushiriki siasa katika chama hicho.
“Mwaka 2000, kulikuwa na mwanamke mmoja katika viti maalumu, mwaka 2005 waliongezeka na kufikia sita na mwaka 2010 wamefikia 26. Mwenyekiti pia ameufanya mwaka huu kuwa wa wanawake kitaifa na ameongeza hamasa ya wanawake kushiriki siasa,” alisema Lymo.
Mbali na viongozi wa chama, alikuwapo pia Sheikh Rajab Katimba kutoka Jumuiya na Taasisi za Kiislamu ambaye alimsifu Mbowe na kuomba agombee tena nafasi hiyo.

Mbowe akubali
Baada ya Mratibu wa Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), Nickson Tugara kummwagia sifa Mbowe, Mapigo Saba alimkabidhi fomu, huku makada wakiimba, ‘Jembe, jembe, jembe…”

Mbowe aliishukuru Kamati Kuu ya chama hicho kwa kupanga uchaguzi Septemba 14, mwaka huu ambayo ni siku yake ya kuzaliwa huku akiahidi kujenga chama imara.

“Mtaiona Chadema mpya ifikapo Septemba 14. Hiki chama hakitakufa na hatutamvumilia mtu yeyote wa kabila lolote atakayekivuruga,” alisema.

Mbowe alisema hajawahi kuomba kugombea uenyekiti wa chama hicho tangu aliponza mwaka 2000…

 “Napata wakati mgumu ninapofikia wakati huu. Chadema ina watu mbalimbali wenye taaluma na uzoefu, kwa nini mimi? Makundi haya yaliyojitokeza kunichukulia fomu yanaweza kutafsiriwa na wapenda majungu kuwa nimepanga mimi.

“Leo ni mara ya tatu naombwa kugombea uenyekiti, sijawahi kuomba. Mwaka 2004, Mzee Makani aliniomba nikamkatalia, lakini akaunda kikundi cha wazee walionichukulia fomu.

“Mwaka 2005, chama hakikuwa na mgombea urais, awali alijitokeza Profesa Mwesiga Baregu lakini akajitoa, nikaambiwa nibebe mzigo. Mwaka 2009 nikaombwa tena kugombea.”

Alisema amedhamiria kujenga chama kimtandao na kimfumo ili kuondokana na mfumo wa kienyeji… “Huko nyuma wakati wa uchaguzi watu walipeana tu nyadhifa kiundugu tukadhani chama kimeongezeka. Lakini wakati huu uchaguzi umefanyika kwa miezi tisa.

“Tulisema hatuwezi kufanya uchaguzi wa Taifa bila kupata viongozi wa mkoa, wilaya, kata, kijiji na mtaa, kitongoji na shina.
 
Tumefanya uchaguzi, watu wamepima na kuona mambo magumu, mara unasikia wanakimbia wakisema wameacha uenyekiti, uache wakati chama kinakua?”

Kondom za MALAYA wa Morogoro Zawaathiri Watoto Wanaoziokota na Kuzifanya Mapulizo

By on 8:51 PM



Biashara ya ngono iliyokithiri katika mji wa Morogoro imegeuka kuwa kero kwa wakaazi wa eneo hilo na familia zao hali inayowaweka hatarini zaidi watoto wadogo wasio na hatia wanaokutana na kondom zilizotumika huku mkuu wa Mkoa huo, Mheshimiwa Joel Bendera akinawa mikono kuhusu suala hilo.

Wakati hayo yakiendelea Morogoro, serikali kuu imekuwa ikitafuta dawa kali ya kuweza kudhibiti biashara hiyo hapa nchini.

Edson Mkisi Jr wa Times Fm, hivi karibuni alitembelea mkoa huo na kushuhudia kushamili kwa biashara ya ngono sehemu mbalimbali za mkoa wa Morogoro hususani katika maeneo ya Kaumba na Itigi mkoani humo.

Taarifa zilizopatikana awali toka kwa baadhi ya wakazi wa maeneo ya mji wa Morogoro zilidai kuwa biashara ya ngono imekuwa kero mkoani humo kutokana na utupwaji hovyo wa kondom zilizotumika katika mitaa hiyo.

Kondom hizo zilizotumika zinahatarisha afya ya watoto wanaozitumia kama mapulizo.

“Kiukweli hii biashara mbali ya kutuaibisha sisi akina mama lakini pia inatukera sana kutokana na utupwaji hovyo wa kondom unaofanywa na hao akina dada….na baada ya kondom hizo kutupwa watoto wetu wanaziokota na kuanza kupuliza kama maputo kwakweli inatukera sio siri,” anasema mama Sakina mfanyabiashara maarufu wa samaki Msamvu Morogoro.

Baadae mwendesha bodabodo eneo hilo alimuonysha mwandishi wetu Hotel moja maaufu na kudai kwamba Hotel hiyo imekodiwa na MALAYA  hao kwa ajili ya kufanyabiashara hiyo na serikali ya mkoa wanatambua ‘ishu’ hiyo!
Advertisement

Polisi amgonga mtoto, Aingia mitini na kutelekeza gari

By on 8:43 PM

Polisi mmoja ambaye hakufahamika jina lake mara moja, aliyekuwa akiendesha gari kwa mwendo wa kasi, Jumapili iliyopita alimgonga mtoto wa kike, Zahara Almeda katika barabara ya Mji Mpya  mkoani  Morogoro.
 
Katika tukio ambalo mwandishi wa habari hizi alilishuhudia, mara tu baada ya kumgonga mtoto aliyekuwa akitoka sokoni kununua magimbi na mihogo, askari huyo aliteremka na kukimbia akiliacha nyuma gari lake lililokuwa bado halijazimwa, ambalo ndani yake kulikuwa na kofia yake.
 
Wananchi waliojawa na hasira baada ya tukio hilo walilizingira gari hilo na kutaka kulichoma moto, lakini busara za baadhi yao ziliwezesha kitendo hicho kutofanyika na baadaye trafiki alifika kudili na tatizo hilo
 
Mmoja wa watu walioshuhudia ajali hiyo iliyolihusu gari aina ya Toyota Baloon lenye namba za usajili T 5** AUE, alisema mtoto aliyegongwa alikuwa akitokea sokoni Mji Mpya, akiwa amebeba kikapu kichwani.
  polisi1
Mtu huyo aliyejitambulisha kwa jina la Sudi Kiwamba, alisema binti huyo alikuwa ameshavuka barabara, lakini wakati akijiandaa kuvuka msingi wa pembeni gari hilo lilimfuata katika jitihada za kumkwepa mwendesha pikipiki.
polisi2
 
Hata hivyo, siku moja baada ya tukio hilo, mwandishi wetu alizungumza na baba mzazi wa mtoto huyo alisema mwanaye anaendelea vizuri na mtu aliyemgonga alikwenda hospitalini kumjulia hali kwani aliamini alikuwa amefariki.

Sunday, August 17, 2014

JIWE Laporomoka jijini Mwanza na kuua Watu Wanne

By on 9:47 PM

Vilio na simanzi jana vilitawala kwa wakazi wa maeneo ya Sinai-Mabatini, baada ya vifo vya watu wanne wa familia mbili tofauti, vilivyotokana na mvua iliyosababisha miamba mikubwa ya mawe kuporomoka na kuponda nyumba zao usiku wa manane. 
 
Tukio hilo la kusikitisha limeripotiwa kutokea saa nane usiku kuamkia jana, wakati mvua   iliyoambatana na upepo wa wastani ilipokuwa ikiendelea kunyesha, na kusababisha miamba hiyo mikubwa inayokadiriwa kufikia tani mbili kuporomoka na kuziponda nyumba hizo na kusababisha vifo hivyo na majeruhi wanne. 
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mlowola, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wananchi kuchukua tahadhari wakati wa mvua.
 
Mpekuzi ilifanikiwa kufika eneo la tukio na kushuhudia miamba hiyo ikiwa imeharibu nyumba, huku nyumba moja iliyojengwa kwa matofali ya tope ikiwa imeanguka na kubaki kifusi.
 
Nyumba zilizokumbwa na maafa hayo zinamilikiwa na watu waliotajwa kwa majina ya Joseph William na Lameck Ajiji, na kila moja watu wawili wamefariki kwa kukandamizwa na miamba hiyo.
jiwe1
 
Katika nyumba ya William iliyokuwa na watu watano, waliofariki wametajwa kuwa ni Kefa Joseph (15) na Emmanuel Joseph (12), wote wanafunzi wa Shule ya Msingi Mbugani na majeruhi mmoja ambaye hakufahamika jina lake ambaye alikimbizwa hospitali.
 
Nyumba inayomilikiwa na Ajiji yenye watu watatu, waliofariki wametambuliwa kuwa ni mama wa nyumba hiyo, Kwinta Geko (24) na mumewe Samson Odinya.
 
Waliojeruhiwa ni mtoto Bety Samson (4) na Godfrey Joseph (14) mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mbugani.
 
Tukio hilo ni la pili kutokea katika eneo hilo la Sinai. Mara ya kwanza ilikuwa ni mwaka 2009 baada ya miamba kuporomoka na kusababisha vifo vya watu wawili wa familia moja.
 
Tukio la jana lilivuta hisia tofauti kwa wakazi wa Jiji la Mwanza, huku wengine wakiangua vilio.
jiwe2
Mamia ya wananchi waliofika eneo hilo, walijitolea kwa kumpa fedha mtoto Bety aliyenusurika kufa kutokana na tukio hilo.
 
Mbunge wa Nyamagana jijini Mwanza, Ezekiel Wenje (Chadema), alifika eneo la tukio na kutoa pole kwa wananchi, ndugu jamaa na marafiki wa familia zilizoathirika na janga hilo, ambapo alionyesha kushtuka baada ya kuelezwa na wananchi kwamba hakuna kiongozi yeyote wa Serikali aliyefika eneo hilo.
 
Akizungumza kwa kutumia kipaza sauti mbele ya umati wa watu waliokuwa wamefurika katika eneo hilo la tukio, alisema: “Inashangaza sana kuona hata mkuu wa wilaya hajafika hapa. Nitawasiliana na viongozi wa Serikali na mchana nitarudi hapa tena.”
 
Baadhi ya wananchi waliozungumza na Mwandishi katika eneo la tukio, waliiomba Serikali kuzuia wananchi kujenga karibu na miamba mikubwa, kwani kufanya hivyo itasaidia sana kuepusha maafa kama hayo.
 
“Kwa kweli tukio hili linasikitisha sana, na tunaomba viongozi wa serikali wasaidie wananchi kuwaondosha kwenye maeneo ya kwenye miamba,” alisema mmoja wa wananchi hao ambaye pia ni balozi wa Shina Namba Tano, Mtaa wa Nyerere A, Jackson Kitundu.

MANGE: Wema Sepetu Badilika, Diamond Yamemfika Shingoni mpaka Anafunguka

By on 9:46 PM

Mange kimambi ambaye ndiye aliyemuibua Wema Sepetu kwa kumshawishi kushiriki Miss Dar Indian Occean 2006 na hatimaye Wema Sepetu kushinda Miss Tanzania 2006 amefunguka kwa kusema kuwa hawezi kumtetea Wema baada ya Diamond kufunguka kuwa Wema anapenda starehe na  ana mashoga wapenda anasa badala ya kujikita kufaya kazi kujiletea amendeleo.
 
Mange amesema kuwa anakubaliana na alichokisema Diamond. Mange ambaye yupo karibu na Wema ameandika .
 
“Mnajua siku zote mimi huwa nakuwa upande wa Wema kwenye issue zake na DIAMOND, Ila leo kwa mara ya kwanza nipo upande wa Shemeji.
 
“Wengi wanalaumu kwanini Diamond aweke hiki kitu hadharani ni kama anamdhalilisha Wema. Jamani nimesoma alichoandika huyu kaka what I can say is he really and truely loves Wema ila Wema mwenyewe anaharibu. 
wema
 
“Yani you can see kabisa he wants the best for his woman ila woman mwenyewe doesn’t want the best for herself. 
 
“Alichosema Diamond ni kwamba yeye kama mwanaume anaweza kumsuport mwanamke wake financially ila kama mwanamke mwenyewe hajisukumi yeye afanyeje sasa? 
 
“Na ameingia deep zaidi kaongelea issue ya mashoga, aisee ! ukiona mpaka mwanaume ameongea hivi tena in public ujue yamemfika shingoni kaona aongee tu. 
 
“Tena you know what this might eventually wake up Wema, ataona duh jamaa kaniambia in private sijaelewa mpaka kaona aongee hadharani bora nibadilike…..Yaani you can see the guy loves Wema soooo much ila kuna vitu vinamboa sanaaaaa na anatamani ambadilishe kidogo. 
 
“The guy mpaka kasema amempa na mtaji wa kufanyia, which is true maana Wema mwenyewe alisema kuwa ile movie(Family) aliyoifanya na Aunty juzi juzi Diamond ndie alitoa mtaji. Hivi nini kingine kaka wa watu afanye muone anampenda demu?
 
“Mimi pia huwa mnanilaumua sana humu simwambii Wema hivi na vile, sijui nini. Ni hivi I respect Wema’s privacy so siwezi kuongea hapa nachoongea nae on a daily basis ili kujitetea kuwa jamani namwambiagaaaaa. Just know , I do talk to her and advice her more than you think.”

Sumaye ashauri kusitishwa kwa Bunge la Katiba

By on 9:45 PM

Waziri mkuu wa zamani nchini Tanzania Fredrick Sumaye amependekeza kusitishwa kwa mjadala wa katiba mpya unaoendelea mjini Dodoma kwa kuwa inaonekana dhahiri kuwa si muda muafaka wa kupata katiba mpya kwa sasa.
 
Amesema kusitishwa kwa mjadala huo kutatoa fursa kwa watanzania kujipa muda zaidi wa kutafakari ili kufanikisha upatikanaji wa katiba muafaka kwa wakati unaofaa.
 
Kauli hiyo ya waziri mkuu wa zamani imekuja wakati bunge hilo linaendelea na vikao vyake mjini Dodoma vinavyohudhuriwa na wajumbe wengi kutoka chama cha Mapinduzi CCM.
 
Wakati huo huo Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), umesema Rais Kikwete ndiye anayeweza kulitolea ufafanuzi suala la kusitisha Bunge Maalum la Katiba na siyo mtu mwingine.
SUMAYE1
 
Umoja huo pia umeendelea na msimamo wa kumtaka Rais kuwasiliana na Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta kulisitisha  bunge  hilo.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Awataka UKAWA Warudi Bungeni…Asisitiza kuwa Rais Kikwete hana Mamlaka kisheria ya Kulivunja Bunge hilo

By on 9:45 PM

Mwanasheria mkuu wa serikali nchini Tanzania Jaji Fredrick Werema amesema hakuna sheria inayompa mamlaka Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kulivunja bunge maalum la katiba hivyo amewataka umoja wa katiba ya wananchi UKAWA kurejea katika bunge hilo kwa lengo la kupata maridhiano ya pamoja.
Jaji Werema amesema hayo jana jijini Dar es salaam wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwa lengo la kufafanua masuala kadhaa yanayohusiana na mwenendo mzima wa Bunge Maalum la Katiba na madai ya umoja wa katiba ya wananchi UKAWA.
Akitumia muda mwingi kufafanua baadhi ya vifungu katika sheria ya mabadiliko ya Katiba, Jaji Werema amesema siyo kweli kwamba Bunge hilo halina mamlaka ya kubadilisha vifungu vya Rasimu, na kusema kuwa kama ingekuwa hivyo, basi kusingekuwa na haja ya kuwepo kwa Bunge hilo.
Kwa kutumia kifungu cha 25 cha Sheria hiyo, Jaji Werema amesema kuwa Bunge hilo limepewa kazi ya kupokea Rasimu, kuijadili, kuiboresha, na kutoa Katiba inayopendekezwa.
Amesema baada ya hapo, litatunga na kupitisha masharti ya mpito na masharti yatokanayo bila kuingiliwa na mtu, kabla ya ukomo wake.
Kuhusiana na madai ya kwamba Rais anaweza kulivunja Bunge hilo, Jaji Werema amesema kuwa Rais hana mamlaka hayo kabla bunge hilo halijamaliza kazi yake na kwamba hakuna mtu yeyote mwenye uwezo huo kwa mujibu wa sheria.
“Hakuna Ugunduzi mzuri uliowahi kufanywa na mwanadamu kama ugunduzi wa Sheria na utawala wa Sheria, hayo ni maandishi tu lakini lazima kila mtu ayafuate” Alisema Werema na kuongeza kuwa..
MWANASHERIA
“Ninamuambia Rais kuwa Rais huna mamlaka ya kusimamisha Bunge la Katiba kwa mujibu wa sheria”
Werema ameongeza kwamba kama lengo la kusitisha vikao vya bunge kwa ajili ya maridhiano, hakuna haja ya kufanya hivyo ka kuwa pande mbili zinazolumbana, kila upande unang’ang’ania maslahi yake, hali inayopelekea kusiwe na dalili za usuluhishi.
SHERIA
Kutokana na hilo, amesema kuwa msuluhishi pekee atakuwa ni mwananchi wakati wa kupiga kura ya maoni na kwamba hivi sasa mjadala wa sura ya Kwanza na Sita umekwisha fungwa.
Werema pia amekiri kuwepo na baadhi ya watu ndani ya CCM wenye mtazamo tofauti lakini hawajasusia Bunge, na kwa kuwa wanafuata misingi ya demokrasia, wakishindwa hoja zao, hukubaliana na hoja zinazoungwa mkono na wengi.

JOHARI Amrushia Dongo IRENE UWOYA….Awachana Waigizaji wa Kike wanaojichia na Kupoteza Mvuto

By on 9:44 PM

Msanii  Johari Blandina ‘Chagula’ ambaye ni star mkongwe Swahiliwood amesema kuwa anamshukuru Mungu kwa kuutunza muonekanio wake na kuwa kama kijana licha ya umri wake kuwa mkubwa tofauti na baadhi ya waigizaji wenzake wa kike ambao hujiachia na kuonekana wazee licha ya umri wao kuwa mdogo.

Akizungumza na Filamucentral Johari alisema:

“Wasanii wa kike wengi ni watoto wadogo lakini kwa sababu ya kujiachia wanaonekana kama watu wazima lakini ukweli ni watoto wadogo sana, namshukru Mungu nimeanza sanaa kitambo lakini mwili wangu upo fiti,”
 
Johari alimtolea mfano Irene Uwoya ambaye ni shoga’ke wa karibu kuwa anaonekana mkubwa kwasasa sababu ya kujiachia licha ya kwamba amempita miaka kadhaa. 
johari
 
Vile vile Johari amesema kuwa kawasasa amerudi kwa moto wa kasi kama muigizaji kama awali baada ya kuwa upande wa producer kuwapa nafasi chipukizi ambao wengi amesema wameshindwa, hivyo amerudi mwenyewe kwenye game.

REPORTED INFORMATION ABOUT EBOLA IN NIGERIA

By on 7:13 AM
EBOLA MIRACLE: Nigerian doctor survives …Discharged 2
BY AZOMA CHIKWE AND JOB OSAZUWA ON AUGUST 17, 2014 · COVER
■ Four others almost fully recovered –Health Minister
The first Nigerian who tested posi­tive to Ebola Virus Disease (EVD) has recovered from the virus and consequently been certified fit and dis­charged, the Minister of Health, Prof Onyebuchi Chukwu told newsmen yesterday in Lagos.
She was one of the doc­tors who had primary contact with the late Liberian Patrick Sawyer while attending to the deceased. Recall that people who had primary contact with late Sawyer, including medics at First Consultant Hospital, Lagos were quar­antined immediately Sawyer tested positive to Ebola virus infection.
The Minister explained that the medical experts at the isolation centre where she was admitted alongside others, have medically monitored the patient, and having fully sat­isfied with her recovery then discharged her home.
“The doctor is safe and free with no risk of infecting oth­ers and had been discharged to go back to her family. In fact, She is even safer than most people on the street who may not know that they have one symptom or the other. Her immunity is boosted and she was closely monitored before being discharged. The experts would have dis­charged her all this while but had to observe her very well because of the nature of the disease,” the Minister said.
He also said that four oth­ers similarly under medical management at the isolation centre were now almost fully recovered from the disease. He also said the other 189 persons, who had secondary contact, were still under sur­veillance in Lagos while ad­ditional six are in Enugu.
Towards arresting fur­ther spread of the disease, the Minister disclosed that patients under treatment were moved to the new 40-bed capacity isolation ward provided by the Lagos State Government at Mainland Hospital, Yaba.
However, the experimen­tal drug, Nano Silver, could not meet the requirements of the National Health Research Ethics Code. Consequently, the National Health Research Ethics Committee withheld approval for it.
Chukwu stated that the experimental drug was made available to the Emergency Operation Centre in Lagos, but was not administered to any patient while awaiting clearance by the Committee.
“However, Chukwu add­ed, “other candidate drugs are currently being evaluated by the Treatment Research Group for EVD. As soon as any of the experimental drugs is cleared by the Committee and is made available, we shall use it in the treatment re­gime subject to the informed consent of the patient.”
So far, out of the 12 people who tested positive, he said four people have died from the dreaded disease.
On the sack of resident doctors, Chukwu confirmed that the suspension is only temporal and that the Federal Government is considering how it can further improve the health care sector.
“I believe the suspension is only temporary, the govern­ment is looking at how the health care system can be im­proved. But please note that the suspension affects only federal-owned hospitals, it is not extended to other state hospitals.”
Recall that that there had been allegations by doctors that the health insurance scheme offered by the federal government had not yet been put in place. The doctors also alleged that health worker who volunteered had not been provided with health in­surance cover by the Federal Government.
Responding to this al­legation, Prof Chukwu ac­knowledged that the Federal Government had indeed not commenced the provisions of insurance policy cover but noted that the Lagos State government has started is­suing the insurance policy to doctors in its employ.
“We are still working on the paper works; when it is ready we would definitely give it out. But we still need more volunteers as health workers are little and they can’t handle the job alone,” he said.
he insurance policy to doctors in its employ.

Ni MaajabU Na Kweli.. Huyu ndiye Baba wa Familia aliyepata ujauzito na kujifungua

By on 6:47 AM
Familia inayoundwa na wanandoa Bianca na Nick Bowser, ni familia yenye furaha lakini iliyowashangaza wengi baada ya Nick ( baba wa familia) kupata ujauzito na kujifungua.

Iko hivi; Nick ambaye ana umri wa miaka 27 hivi sasa, alizaliwa na jinsia ya kike na kupewa jina la Nicole na wazazi wake, lakini aliamua kubadilika na kuishi kama mwanaume (transgender/jike dume) tangu miaka saba iliyopita. Na hii ilichangiwa pia na sura na umbo la kiume alilokuwa nalo.

Hali ilikuwa hivyo pia kwa Bianca ambaye ana umri wa miaka 32 hivi sasa, yeye alizaliwa mwanaume na kuitwa jina la Jason, lakini kutokana na kuwa na sura nzuri na umbo la kike, na hisia zake za kutaka kuishi kama mwanamke, alibadili aina ya maisha na kuishi kama mwanamke kamili.

Wawili hao walikutana na kuamua kufunga ndoa huku wakiyabadilisha kabisa maisha ya wana ndoa, Nick akiwa baba wa familia anaevaa na kuishi kama mwanaume. Mkewe Bianca (ambaye ni mwanaume) yeye alibadili na kuishi kama mwanamke kamili akiihudumia familia yake na kuvaa mavazi ya kike kama mama siku zote.

Lakini kwa mujibu wa Bianca, wawili hao wamekuwa wakishiriki tendo la ndoa kama kawaida kwa kuwa wanaamini kubadili kwao mfumo wa maisha hakuwezi kubadili viungo vyao vya mwili. Matokeo yake, baba alipata ujauzito na kujifungua. Na hivi sasa wana watoto wawili.

Cha kushangaza ni kwamba wana ndoa hao hawawachanganyi majirani tu, lakini pia wamewaficha hadi watoto wao wadogo ambao wanaamini kabisa kuwa Bianca ndiye aliyewazaa na baba yao ni Nick. Lakini siri hii itakaa hadi lini ili hali majirani wanajua na wa wanandoa hao wameshaeleza kwenye vyombo vya habari?

“Sifahamu lini tutaanza kuwaambia ukweli, labda wakati ambapo Kai (mtoto wao mkubwa) atakapokuwa na miaka sita hivi, lakini wanatakiwa kuwa na umri mkubwa wa kutosha kuelewa. Ni muhimu wakifahamu kwa kuwa ni siri kubwa ya kuwaficha watoto wako na kama wakifahamu kupitia njia nyingine watachukia sana.” Alisema Bianca.


Biana aliendelea kujitetea kuwa kuwa jike dume/ dume jike haielezi jinsi ulivyo. Ni kama kuwa na rangi nyeupe, nyeusi, mnene au mwembamba haielezi kitu kuhusu jinsi ulivyo.

Kwa upande wa Nick, anasema mara ya kwanza alipopata ujauzito wa Kai alibadilika na kuishi kama mwanamke, hivyo ikawa kama yeye na mumewe wote ni wanawake. Wengi walidhani wanacheza mchezo wa kusagana.

Lakini alipopata ujauzito wa pili ndipo alipoamua kuishi maisha yake ya kawaida kama baba na kitumbo chake. Hali ilimnyima raha mbele za watu waliokuwa wanamshangaa sana.

“Lakini, nilipokuwa na ujauzito wa Pax (mtoto wa pili), watu walikuwa wananishangaa sana, kitu kilichonifanya nikose ujasiri. Sikuweza kuvumilia hali ile, watu kunong’onezana wakiniona, kuninyooshea video na mwisho nikawa siwezi kutoka nyumbani. Nilitoka kwenda kumuona daktari tu. Watu waliogopa kile wasichokifahamu.” Alisema Nick.

Naye Biance alipoulizwa kuhusu suala la kufanya mapenzi, hakusita kueleza wanavyoichukulia.

“Tunaviungo vyote kwa hiyo tunavitumia. Kama tungeweza kuvibadili tungefanya hivyo, ni ingekuwa tofauti- lakini hatuwezi na watoto wanakuja kwanza.”

Sasa hii tunaiitaje? Kila mmoja anatafsiri yake, kwa imani yake na uelewa wake pamoja na mila na desturi. Maajabu hayaishi! kwa lugha ya kiingerza tunaiita category ya Life Styl

Utabiri wa Askofu Kakobe Unaendelea Kutimia: Ikulu na Mwanasheria wa Serikali watofautiana

By on 6:24 AM

Ni mazingaombwe yanayoweza kupatikana tanzania pekee duniani.
‘ikulu inatoa tamko lao kuwa bunge litaendelea na katiba lazima ipatikakane bila hata ya kuwepo umoja wa katiba ya wananchi [ukawa].
Na wakati huo mwanasheria mkuu wa serikali anakuja na vituko vingine vya kuueleza umma wa watanzania kuwa bila [ukawa] katiba mpya haiwezi kupatikana.na tena anaenda mbali kwa kuwaomba kwa moyo mweupe na kiunyenyekevu wale aliowaita matumbili,ati tu kwa sababu wanapigania maslahi ya umma wa watanzania kuwa ame miss manjonjo yao ya kupigania ukombozi wa watanzania!
kakobe
-hapa tukubali tukatae lazima kutakuwa na ombwe la uongozi nchini.
Na askofu zackari kakobe atashinda kwa unabii wa maneno yake kuwa c.c.m itasambaratika katika ramani ya dunia na hatutaiona wala kuisikia tena!

Alikiba: Nawaomba watu Wasinikosanishe na Diamond, Sina Ugomvi Naye

By on 6:12 AM

Alikiba anataka watu wafahamu kuwa hana na tatizo na Diamond Platnumz na amewataka watu waache kuwakosanisha.

Akizungumza na Bongo5 leo, AliKiba amewataka watu kuachana na tabia ya kuwagombanisha Diamond ili wafanye muziki mzuri.

“Kila mtu anaandika anachotaka juu ya mimi na Diamond, mpaka wengine wanatumia akaunti fake za Facebook kutukosanisha, ndio maana nikasema kuna wengine wanafanya for fun na wengine wanafanya ili kutukosanisha wengine wanafanya lakini hawajui wanachofanya,” amesema Alikiba.
alikiba

“Mimi najaribu kuwaomba wadau mbalimbali waache hiyo tabia ya kutukosanisha kwa sababu mimi sina ugomvi na Diamond na wala sina mambo hayo. Ninachowataka waendelee kusupport kazi zetu ili mambo yaende vizuri kwa sababu sisi ndo wasanii wao tunaoiwakilisha Tanzania. Wanapotupa moyo wao sisi tunazidi kukaza buti ili tufike mbali zaidi. Watu wanaotengeneza ugomvi wangu na Diamond waache cha zaidi wafanye kusupport muziki na watuambie ni mapungufu gani ambayo yamepungua ili tujirekebishe,” ameongeza.

Katika hatua nyingine, Alikiba amezungumzia mapokezi ya wimbo Mwana na Kimasomaso pamoja na ujio wa video zake.
Diamond Platinumz
Diamond Platinumz

“Kwanza watu wamenipokea vizuri sana kama nilivyokuwa nikitarajia, imeonyesha ni jinsi gani yale malalamiko ya maana walikuwa wakilalamika kwamba nimekumiss na nilivyotoa nyimbo watu wanasikiliza na kuinjoy na nyimbo zenyewe zimekuja wakati mzuri na zenye maadili mazuri ya kuelimisha na kuchezeka na ya kufurahisha. Maandalizi ya video yapo tayari na booking ipo tayari vilevile, maandalizi nimeandaa hata kabla sijatoa nyimbo, video itafanyika nje na moja ni hapa siwezi sema ni nchi gani bado ni mapema nitasema baadae nikishaitoa, kwasababu nimetoa track mbili moja itafanyika hapa na nyingine itafanyika nje.”