Saturday, May 3, 2014

Huyu ni shemeji yangu kabisa, mke wa kaka yangu....Lakini utani wake umepitiliza....Nipeni ushauri

By on 11:32 PM

Kuna ule utani wa mashemeji lakini utani wa shemeji yangu huyu umezidi ndugu zangu. Siku moja nilikuwa natoka zangu kwenye mizunguko yango ya kila siku mjini, nilipofika nyumbani nilimkuta shemeji yangu nyumbani,  kaka alikuwa bado hajarudi. kama kawaida yake akaanza.

“Haya mume wangu kipenzi leo umeniletea nini” Nikamwambia leo sina kitu wife kesho nitakuletea bonge la zawadi ,akasema wala usijali mume wangu leo nina bongo la zawadi yako, mi nikajua utani...!!
 
Aliniacha sebuleni yeye akaingia chumbani kwake na mimi pia sikukaa sana nilienda chumbani kwangu.Mara tu nikasikia ananiita "shemeji njoo huku tayari", nikatoka, akaniambia njoo huku chumbani kwangu, nikafika ila nikaishia mlangoni akaniambia ingia shemeji.

Nilipoingia  nikamkuta amevaa nguo moja fupi ya ajabu ...akaniambia ngoja nikuonyesha mambo ninayompa kaka yako.Akaanza kukaa style tofauti tofauti pale kitandani za kusisimua, kweli nilishindwa kumuelewa nikamuuliza shemeji huu ni utani pia au uko serious??.
Akaniangalia tu machoni halafu akaendelea. Nilivyoona vile nilifungua mlango nikatoka. Akaaniita kwa hasira mi nikarudi chumbani kwangu nikalala. 

Sasa naona  hata aibu kumwangalia shemeji yangu. Hii ni sawa kweli wadau??..

0 comments:

Post a Comment