Saturday, August 16, 2014

NDANI YA HABARI: Watoto 11 chumba kimoja, watumikishwa kuuza vitumbua

By on 12:07 AM
“Hao watoto hatujawaiba, tumewatoa kwao huko mikoani na biashara wanazofanya ni hizo ndogondogo wala siyo ngumu. Wengine hapa hawana baba wala mama wanazunguka tu mitaani. Wameona kuliko kuiba, ni bora waje wafanye kazi ili wapate pesa za kujikimu,” anasema Fatuma. 
Na Elias Msuya, Mwananchi

  • Mmiliki wa biashara hiyo asema alifanya hivyo kuwasaidia kwa kuwa wazazi wao hawana uwezo wa kuwasomesha.


Pengine takwimu za Umoja wa Mataifa (UN) kwamba watoto wapatao milioni 250 wanatumikishwa katika ajira mbalimbali duniani kote, zikawa ndogo kulingana na hali halisi kwa kuwa kila kukicha, mapya huibuka.
Ajira hizi zinapaswa kupigwa vita kwa kuwa siyo tu zinawanyima haki za msingi watoto, bali zinachochea umaskini kwa familia na taifa kwa jumla.
Hassan Abdallah mkazi wa Tabata ni mmoja kati ya wanaoshiriki katika biashara hii haramu ya kuajiri watoto. Hivi sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kuajiri watoto 11 kwa kazi za kuuza vitumbua huku akiwahifadhi ndani ya chumba kimoja.
Kati ya waajiriwa hao, watoto walio chini ya umri wa miaka 18 wako wanane.
Katika makazi hayo, watoto walimwonyesha mwandishi wa habari hizi banda la mabati wanalotumia kwa malazi likiwa kando ya nyumba ya mwajiri wao.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kisukuru, Lukresia Msuya anasema kuwa Abdallah na mkewe Fatuma Shomari wamekuwa wakiwafuata watoto hao mikoani na kuwaleta jijini Dar es Salaam kuwatumikisha kuuza vitumbua mitaani.
“Tulipigiwa simu juzi na katibu wa CCM wa mtaa akisema kuwa kuna jambo la muhimu. Hapo ndipo aliponionyesha nyumba hii ambayo ina watoto wanaotumikishwa kuuza vitumbua. Tukawakusanya na kuwapelekapolisi,” anasema Msuya.
Amewataja watoto wanaoishi kwenye nyumba hiyo kuwa ni pamoja na Furaha Samuel, Steven Tudius, Amani Adison, Yusuf Simon, Richard Zakaria, Kackson Jackson Michael, Elia Wilson, Boniface Lawrence, Baraka Francis, Zamda Yumpunju, Jema Ramadhani na Haji Ramadhani.
Msuya amesema kuwa baada ya kupata taarifa hiyo, walikwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi cha Kisukuru kisha kuhamishia shauri hilo Stakishari ambako Abdallah aliwekwa ndani.
“Nikiwa kama mzazi inaniuma kuona watoto hawa wadogo wenye umri kati ya 17 na 12 wakifanyishwa kazi kama hizi. Nawaomba wazazi wawakumbatie watoto kama vifaranga vya kuku. Mtoto wa miaka 12 umfanyishe kazi, halafu utamlipa nini kama siyo kumdhulumu?” alihoji.
Jinsi walivyokamatwa
Akieleza jinsi alivyogundua suala hilo, katibu wa CCM wa Mtaa wa Kisukuru, Thomas Matiku anasema kuwa alipewa taarifa na wananchi wakati akitoka Buguruni.

0 comments:

Post a Comment