Friday, August 15, 2014

RAIS KIKWETE AWAAPISHA MAJAJI WAPYA 20 WA MAHAKAMA KUU YA TANZANIA IKULU JIJINI DAR

By on 11:41 PM

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu pamoja na Majaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania na Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wapya.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali, Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda, Waziri wa Sheria na Katiba Dkt Asha-Rose Migiro, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman Makungu, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, Mwanasheria Mkuu Jaji Frederick Werema, Mtendaji Mkuu wa Mahakama Mhe Hussein kattanga katika picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama kuu ya Tanzania baada ya kuapishwa leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu pamoja na Majaji wa Mahakama ya Kuu Tanzania na Majaji wapya.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu pamoja na majaji wapya.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu na Jaji Kiongozi Shaban Ally Lila wakiwa katika pic ha ya jumla na Majaji wapya na wa zamani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete asubuhi ya leo, Ijumaa, Agosti 15, 2014, amewaapisha Majaji 20 wapya wa Mahakama Kuu ya Tanzania ambao aliwateua mwanzoni mwa wiki hii katika hafla iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam.
Halfa hiyo iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam ilihudhuriwa pia na Makamu wa Rais Mheshimiwa Mohamed Gharib Bilal, Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda, Jaji Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Mohamed Chande Othman, Waziri wa Katiba na Sheria Mheshimiwa Asha Rose Migiro na Jaji Mkuu wa
Zanzibar Mheshimiwa Omar Othman Makungu.
Majaji hao wapya wa Mahakama Kuu ya Tanzania ni pamoja na akinamana wanane na uteuzi
huo wa Mheshimiwa Rais Kikwete umeshirikisha wanasheria kutoka Serikalini, Taasisi za Umma, Jumuia ya Afrika Mashariki, Sekta Binafsi na Asasi za Kiraia.
Majaji hao wapya ambao wameapishwa leo ni Jaji Penterine Muliisa Kente, Jaji Benedict Batholomew Mwingwa, Jaji Eliezer Mbuki Feleshi, Jaji John Eudes Ruhangisa, Jaji Winfrida Beatrice Korosso, Jaji Lilian Leonard Mashaka, Jaji David Eliad Mrango, Jaji Edson James Mkasimongwa, Jaji Mohamed Rashid Gwae na Jaji Firmin Nyanda Matogoro.
Wengine ni Jaji Leila Edith Mgonya, Jaji Barke Mbaraka Abdou Sehel, Jaji Awadhi Mohamed, Jaji Lugano J. Mwandambo, Jaji Rose Ally Ibrahim, Jaji Paul Kihwelu, Jaji Modesta Opiyo Makopolo, Jaji Amour Said Khamisi, Jaji Mary Caroline Levira na Jaji Salma Maghimbi.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
15 Agosti, 2014

0 comments:

Post a Comment