Saturday, August 16, 2014

Steve Nyerere kugombea ubunge jimbo la Kinondoni mwaka 2015

By on 1:07 AM

Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steve Nyerere ametangaza nia yake ya kugombea ubunge mwaka 2015 katika jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam kwa kupitia tiketi ya CCM.
Mwenekiti wa bongomovie Steve Nyerere
Mwenekiti wa bongomovie Steve Nyerere
Akizungumza na Bongo5, Steve Nyerere amesema yupo kamili na amejipanga kufanya hivyo ifikapo mwakani.
“Ukiona chereko chereko ujue mambo yameiva, yeah nitagombea ubunge mwakani. Nimejipanga na ninaweza kufanya hivyo, nipo vizuri sana,” amesema.
Katika hatua nyingine Steve Nyerere amewakaribisha watanzania wote hapo kesho katika shughuli maalum ya kuwaombea wale waliotangulia mbele ya haki itakayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam kuanzia saa 4 asubuhi.

1 comments: