Sunday, July 6, 2014

KAMPENI YA TOHARA YA WANAUME YAZIDI KUSHIKA KASI MKOANI IRINGA

By on 4:39 AM



Licha ya elimu ya kampeni za tohara  katika wilaya ya kilolo kupokelewa na    kuwa na  mwamko wa kujitokeza  kwa watu kwa kiwango kikubwa katika zoezi la kufanyiwa tohara  bado kunachangamoto zinazowakumba watoa huduma katika kituo cha kutolea huduma hiyo.

Akizungumza mwelimishaji rika wa kampeni za tohara zinazoendeshwa na shirika lisilo la kiserikali la JPIEGO kutoka katika kituo cha afya cha nzihi SCOLASITIKA MKWEMWA amesema kuwa watu kuanzia 98 mpaka 99 hujitokeza kwa siku.

Amema kuwa,kuna wakati wamekuwa wakishindwa kuwahudumia na kulazimika kusitisha huduma kutokana na kuwa jengo husika halina umeme, kwani huduma hizo hufanyika hata nyakati za usiku.

Amesema kuwa wengi wao wanapenda kupewa huduma hiyo mida ya usiku kwa ajiri ya usiri huku akiitaja  changamoto nyingine kuwa ni watu wanashindwa kujitokeza kutokana na kuwa huduma hiyo inaambatana na zoezi la upimaji vvu.

Akizungumza meneja wa eneo hilo DOLIC KADETE amesema kuwa huduma ya tohara kwa kituo hicho huanza saa 2 asubuhi hadi saa kumi na moja jioni.

Ameongeza kwa kutaja changamoto nyingine inayowakabili ni kuwa asilimia kubwa ya watoto wanaorudishwa kwa ajili ya kuangaliwa maendeleo ya vidonda huwa haviko katika hali nzuri.

Akizungumza mmoja wa  wanaume ambao wamefanyiwa tohara KASIANI SAFARI amelishukuru shirika la jpiego kwa huduma hiyo huku wakiwashauri wanaume wengine ambao hawajafanyiwa tohara kujitokeza kupata huduma hiyo kwani itawasaidia kuwakinga na magonjwa ya zinaa.

 Kampeni za tohara zinafanyika katika mikoa ambayo kiwango cha maambukizi ya vvu kiko juu na katika mikoa ambayo tohara inafanyika kwa kiwango kidogo kuanzia miaka 10 na kuendelea Lengo likiwa ni kusaidia kupunguza maambukizi ya vvu kwa asilimia 60.

Aidha kampeni za tohara ambayo ni kuanzia mwezi wa tisa mwaka jana hadi mwezi wa tisa mwaka huu shirika la jpiego lilipanga kuwafikia watu laki moja na ishirini na tano elfu na kufikia mwezi huu wa saba tayari wameshafikia lengo.

0 comments:

Post a Comment