Wednesday, July 9, 2014

TIMBWILI ZITO ..... MCHEPUKO WAMTOKEA PUANI MUME WA MTU, SHUHUDIA MWENYEWE HAPA

By on 3:15 AM

Bw. Paulo Ndulu akijaribu kuamua ugomvi kati ya mkewe, Anitha Mapunda na Elizabeth Chacha (mwenye shati nyekundu) anayedaiwa kuwa ni hawara yake.

KUNA matukio ambayo kama binadamu yasikie kwa wengine tu lakini yasikutokee wewe! Kama hili la mkazi wa Ukonga –Mzambarauni, Dar, Paulo Ndulu ambapo mkesha wa kuamkia Sikukuu ya Sabasaba, alijikuta katika wakati mgumu pale alipoingia kibaruani kuamua ngumi kati ya mkewe, Anitha Mapunda na Elizabeth Chacha aliyedaiwa kuwa ni hawara yake, OFM walishuhudia.OFM ni kikosi cha kifichua maovu cha Global Publishers ambacho katika kipindi hiki cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan kimekuwa kikizunguka usiku ili kuhakikisha hakuna watu wanaokwenda kinyume na swaumu za Waislam.

0 comments:

Post a Comment